Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 1 of 42
This booklet on Sexually Transmitted Infections was developed by the Tanzania Home
Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and
more information on the project are available at
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania.
MAGONJWA YANAYOAMBUKIZWA KWA NJIA YA NGONO
Kila mwanamke ana haki ya kufurahia tendo la ngono bila woga wowote
wa kupata maradhi. Ina maana ya kwamba tunahitaji kujua jinsi ya kujikinga
wenyewe dhidi ya magonjwa ya zinaa, jinsi ya kutibiwa kama tukiambukizwa,
na jinsi ya kuepuka kueneza uambukizo bila ya kuacha kufanya ngono.
Kwa sababu kuenea kwa ugonjwa wa UKIMWI kumewafanya watu wengi
kujitambua, watu wengi sasa hivi wako tayari kuzungumzia kuhusu matumizi ya
mipira ya kiume – kondom na njia nyingine za kujikinga ili kuepuka kupata virusi
vinavyotishia maisha ya watu wengi. Lakini kuongelea kuhusu hatari ya kupata
ugonjwa na kukubaliana kufanya ngono salama bado ni jambo gumu
kulitekeleza. Watu wengi wanaelewa vizuri juu ya hatari za uambukizo wa
magonjwa ya ngono, lakini hawatumii mipira ya kiume au kinga zingine. Kwa
sababu magonjwa ya njia ya ngono yako sana, na kwa sababu mengi
hayaonyeshi dalili wengi wa watu wana kuwa hana habari kuwa wana ugonjwa.
Pia kwa sababu ya uelewa katika kijamii kuhusu tendo la ngono, kuwa na
ugonjwa wa aina hii kunaweza kuukakuletea aibu, hasira na msongo wa
mawazo. Tunaweza kujihisi kuwajibika na kujilaumu wenyewe kusikostahili.
Inaweza kusaidia kama tukikumbuka kwamba magonjwa ya zinaa ni matatizo ya
kiafya kama mengine.
Nilipogundua kwamba nina uambukizo wa virusi vya Papiloma HPV (Human
Papiloma Virus) Nilisikitika sana ……… Nakumbuka jinsi nilivyokuwa naogopa
kumwelezea mwenzi wangu mpya kuhusu ugonjwa huo. Naye alisema “Niko
tayari kuishi na huo ugonjwa”. Sikuacha kuwasiliana naye. Kitendo hicho kilinipa
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 2 of 42
moyo kuwa ninaweza kuendelea kufanya ngono katika maisha yangu kama
kawaida hata kama nina matatizo haya ya kiafya.
Kama mtu ana mpenzi mmoja halafu akapata ugonjwa wa zinaa atakuwa
ameambukizwa kwa njia ya ngono ya kutoka nje ya uhusiano wao. Kwa hiyo
basi, uambukizo huo huleta mfarakano mkubwa ndani ya ndoa.
Mume wangu aliniambia kwamba alishiriki tendo la ngono na mtu mwingine na
anaweza kuwa ameambukizwa ugonjwa wa zinaa. Sikujua nini cha
kufanya…jana nililiona tangazo moja la biashara kwenye mtandao linalohusu
ugonjwa wa zinaa, baada ya kusita sana, niliamua kuwasiliana nao. Nilipata
ahueni baada ya kupata ushauri bila ya mtu yeyote kunitambua nilikuwa nani.
MAGONJWA YA ZINAA NI YAPI?
Magonjwa ya zinaa ni istilahi inayotumika kwenye magonjwa mengi ambayo
huambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya ngono
ya ukeni, mdomoni au njia ya haja kubwa. Maambukizo mengi yanaweza
SIDEBAR
Kujifunza zaidi kuhusu kuzuia maambukizo ya magonjwa ya zinaa, Tazama sura ya 14, “Ngono
salama.”
END SIDEBAR
kuenea kwa njia ya ngono, lakini baadhi tu ni ya kawaida nchini Marekani.
Pamoja na VVU, magonjwa haya ni kama chlamydia, kisonono, kaswende,
kutokwa na malengelenge sehemu za siri, Human papilloma virus, (HPV),
ugonjwa wa homa ya manjano, Trikomoniasis (kutokwa na maji maji yenye
harufu ukeni na bacterial vaginosis (BV).
MAGONJWA YA ZINAA YANAAMBUKIZWAJE?
Magonjwa ya zinaa huambukizwa haswa kupitia kwenye damu, manii, majimaji
yatokayo ukeni, na uchafu utokao kwenye vidonda au michubuko
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 3 of 42
inayosababishwa na kufanya ugonjwa utokanao na ngono. Njia kubwa ya
kuambukizwa ugonjwa wa zinaa ni kufanya ngono ya ukeni, mdomoni na kupitia
njia ya haja kubwa bila ya kutumia kinga. Pia unaweza kuambukizwa kwa
kugusana sehemu zingine za mwili zenye vidonda na michubuko, au kwa
kuchangia vifaa vyenye ncha kali kama nyembe, sindano, au kifaa cha bandia
cha kufanyia ngono, kama kitakuwa na maji maji ya mwilini kutoka kwa mtu
mwingine. Baadhi ya magonjwa ya zinaa kama, malengelenge yanaweza
kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa kugusana
ngozi. Uwezekano wa kupata magonjwa ya zinaa kupitia matumizi ya vyoo vya
kukalia au taulo sio rahisi. Kuongezewa damu au kupandikiza kiungo cha mwili
wa mtu mwingine kunaweza kupata uambukizo kama damu na kiungo hicho
haitachunguzwa vizuri ili kubaini ugonjwa, hata hivyo uchunguzi makini
umeanzishwa na kutumiwa nchini Marekani.
KUNA UHUSIANO GANI KATI YA VVU NA MAGONJWA MENGINE YA
ZINAA?
Uambukizo wa ugonjwa wowote wa zinaa unatufanya tuwe kwenye hatari zaidi
ya kupata VVU, kirusi ambacho husababisha UKIMWI kama tutaambukizwa.
Kwanini? Maambukizo ya ugonjwa unaotokana na ngono huweza kusababisha
kuchanika kwa ngozi, vidonda, au michubuko kwenye sehemu za mwili ambazo
ziko kwenye hatari ya kupata uambukizo wa VVU kama Uke, na kufanya iwe
rahisi zaidi kwa virusi kuingia kwenye mishipa ya damu. VVU hushambulia hasa
seli nyeupe za damu, ambazo hukinga mwili dhidi ya magojwa, kwa hiyo
unapokuwa una uambukizo wa ugonjwa wa zinaa mwili kutengeneza seli hai
nyeupe nyingi za damu na hivyo kushambuliwa na VVU. Mwishowe, tabia
hiyohiyo hatarishi ambayo inaweza kutusababishia kuambukizwa ugonjwa
mmoja pia huongeza uwezekano wa kuambukizwa magonjwa mengine na
mwenzi mwenye ugonjwa mmoja wa zinaa huweza kuwa na magonjwa mengine.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 4 of 42
Na jinsi ya kujikinga dhidi ya magonjwa ya zinaa, Tazama “Ukimwi sura ya 16”
UONGO AU UKWELI?
Ninaweza kuambukizwa ugonjwa wa zinaa kwa kufanya ngono ya mdomoni.
Ukweli: Ngono ya mdomoni inahusisha na kubadilishana majimaji ya mwilini
ambayo huweza kusababisha maambukizo. Wakati mwenzi wako anapofanya
ngono ya mdomoni na wewe, au wewe unapofanya ngono ya mdomoni na
mwanamke mwingine, unatakiwa utumie mpira maalum wa mdomoni ili kuzuia
maambukizi kupitia majimaji ya mwilini. Na kama mwenzi wako ni mwanaume,
anatakiwa avae mpira wake wa kiume- kondom kabla mdomo wako haujagusa
uume wake.
• Kama nitaambukizwa ugonjwa wa zinaa, dawa zitaweza kunitibu haraka.
uongo: Virusi vya magonjwa ya zinaa kama malengelenge, ugonjwa wa
manjano, HPV, na VVU vinaweza kutibiwa na kupunguza maumivi na kupunguza
kuendelea kwa maambukizi, lakini uambukizo kamwe hautatibika. Magonjwa ya
zinaa kama Chlamydia, kaswende na kisonono ambayo husababishwa na
bakteria, protozoa, na vijidudu wengine wadogo yanaweza kutibiwa kwa dawa
za kumeza au kupaka. Hata hivyo “kutibika” kunamaanisha ya kwamba
kuendelea kwa uambukizo kunakomeshwa kabisa; lakini madhara yaliyotokea
kwenye mwili wako hayawezi kurekebishwa kabisa
Kwa hiyo, kujikinga dhidi ya magonjwa yote ya zinaa kunasaidia kujikinga na
VVU. (kwa maelezo zaidi kuhusu VVU, tazama sura ya 16, “VVU na UKIMWI.”
DALILI ZA MAGONJWA YA ZINAA NI ZIPI?
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 5 of 42
Dalili za kawaida za ugonjwa wa zinaa ni:
• Kuhisi maumivu au kuungua wakati wa kukojoa.
• Kuwashwa, kutokwa na uchafu au harufu isiyokuwa ya kawaida ukeni,
kwenye uume au njia ya haja kubwa.
• Kwa wanawake hupata maumivu makali chini ya tumbo (kinena).
• Kuwa na uvimbe, vidonda au vipele mara nyingi kuzunguka sehemu za
siri au eneo la njia ya haja kubwa.
Mara nyingi dalili hutokea kwenye maeneo ya sehemu za siri. Wakati
mwingine huathiri pia mapaja, koo, na macho (dalili hizi ni kawaida kwa ugonjwa
wa kisonono), mdomoni (kwa ugonjwa wa kaswende na malengelenge), au sio
mara nyingi, kwenye pua na mikono. Dalili za mwanzo za kaswende ni kupata
vidonda visivyokuwa na maumivu au visivyoeleweka (kama upele ambao
hutokea kwenye hatua ya pili). Kwa sababu havina maumivu na haviendelei,
wengi wetu hatuwezi kutambua kama tayari tumeshapata maambukizi ya
magonjwa haya. Dalili hizi huweza kupotea zenyewe kabla hatujaingiwa na hofu,
hivyo uambukizo ukaendelea kusambaa kwenye miili yetu.
BAADHI YA MAGONJWA YA ZINAA HAYAONYESHI DALILI ZOZOTE:
Wanawake wengi wanaopata uambukizo wa ugonjwa wa chlamydia huwa
hawatambui kwamba wana tatizo lolote. Vivyo hivyo kwa ugonjwa wa kisonono
ambao mara nyingi hauonyeshi dalili pia. Kama magonjwa haya hayatatibiwa
yanaweza kuleta madhara makubwa kwenye njia ya uzazi yanayoitwa ugonjwa
wa uvimbe kwenye via vya uzazi (inflammatory disease -PID). Hata hivyo,
maambukizi haya ya bakteria yanatibika kabisa, na madhara yake pia yanaweza
kuzuilika (tazama, sura ya 28, “Ni Pekee kwa wanawake”
KAMA NINA DALILI MOJAWAPO KATI YA HIZO, JE NINA UGONJWA WA
ZINAA?
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 6 of 42
Sio kila wakati. Ni muhimu kuchunguza nini kinachosababisha. Ingawa inaweza
kuwa ni kitu kingine kabisa, lakini usizipuuzie hizo dalili. Haya maambukizi
yanatakiwa kuchunguzwa na kutibiwa.
Kuvimba kwa ngozi ya uke na sehemu ya nje ya uke kunaweza kusababishwa
na vitu vingi. Kitu cha kwanza ni kubadilika kwa pH (uwiano wa asidi na alkalini)
ndani ya uke. Vitu ambavyo vinaweza kuathiri pH ni pamoja na manii (ambayo
hupunguza kiwango cha asidi ukeni), kusafisha uke kwa maji au vitu vingine,
hedhi, na aina zingine za maambukizo. Dawa (Kiua vijasumu) zinaweza kuua
baadhi ya vijidudu muhimu kwenye uke, na hivyo kuruhusu vijidudu vingine kama
fangasi kukua zaidi. Wanawake wengine hutokwa na uchafu ukeni bila sababu
yoyote ya kueleweka. Kujamiiana mara kwa mara kunaweza kufanya
maambukizo ya ukeni kuwa na madhara makubwa zaidi, kwa sababu vijidudu
vya maradhi husukumwa zaidi kuelekea ndani zaidi ukeni. Kemikali katika
vipodozi au hata nguo vinaweza kusababisha mwasho.
Maambukizo ya kwenye njia ya mkojo (UTI), ni pamoja uvimbe uliojaa
maji, unaweza pia ukaonyesha dalili. Uambukizo wa njia ya mkojo huweza
kutokea kwa kujamiiana au bila kujamiiana. Tunaweza kupata maabukizo kwa
vijidudu kutoka kwenye njia ya haja kubwa au eneo la njia ya haja kubwa kwenda
kwenye njia ya mkojo na Kibofu cha mkojo - tunapofanya ngono ya ukeni baada
ya kufanya ngono kupitia njia ya haja kubwa, au tunapojifuta/jitawaza kutoka
nyuma kuelekea mbele. Uvimbe-“Honeymoon cystitis” hutokea wakati wa
kujamiiana ambapo manii husukumwa kuingia kwenye njia ya mkojo.
MAGONJWA YA ZINAA YANATIBIKA?
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika. Magonjwa ya zinaa yanayosababishwa na
bakteria protozoa, na vijidudu vingine yanaweza kutibiwa kwa kumeza dawa
(kiua vijasumu) au kupakaa krimu na losheni. Magonjwa ya zinaa ya aina hii ni
pamoja na kaswende, chlamydia; kisonono, na trichomaniasis. Orodha hii pia
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 7 of 42
inajumuisha vimelea wa kwenye ngozi kama utitiri, ukurutu ambao husababisha
mwasho, kutokwa na vipele na huweza kuambukizwa kwa njia ya ngono.
“Kutibika” inamaanisha kwamba vijidudu vinaweza kuuawa na kukomeshwa
ueneaji wa uambukizo. Ila haimaanishi kwamba madhara yaliyotokea yanaweza
kuondolewa. Uambukizo usiogundulika na kupatiwa matibabu unaweza kuwa na
madhara mabaya sana. Kinga ni bora zaidi kuliko tiba, na kuwahi mapema
matibabu baada ya kuona dalili huepusha madhara ya muda mrefu.
Virusi vya magonjwa ya zinaa vinaweza kutibiwa lakini haviwezi kuponywa.
Virusi vya kawaida vya magonjwa ya zinaa ni pamoja na vya malengelenge,
homa ya manjano B, virusi vya papilloma (HPV), ambavyo husababisha uvimbe
kwenye uke na mabadiliko mengine kwenye seli za mlango wa mji wa mimba na
virusi vya UKIMWI (VVU) ambavyo husababisha UKIMWI. Matibabu husaidia
kutibu dalili za ugonjwa na kupunguza kuendelea kuenea kwa maambukizo ya
virusi lakini sio kuwaondoa /kuwaua virusi
UWEZEKANO UKOJE WA KUAMBUKIZWA UGONJWA WA ZINAA?
Magonjwa ya zinaa ni miongoni mwa magonjwa ya kawaida ya kuambukiza sasa
hivi nchini Marekani. Zaidi ya watu milioni 65 katika nchi hii hivi karibuni wana
maambukizo ya ugonjwa wa zinaa usiotibika. Kila mwaka zaidi ya watu milioni 18
hupata maambukizi` ya magonjwa ya zinaa wa aina moja au zaidi, na zaidi ya
nusu ya maambukizi mapya ya ugonjwa wa zinaa hutokea kwa watu kuanzia
wenye umri wa miaka kumi na mitano hadi ishirini na minne1. Kama tutafanya
ngono zembe na mtu ambaye tayari ana ugonjwa wa zinaa au kama sisi tayari
tumeshaambukizwa, tuna uwezekano mkubwa wa kuambukizwa ugonjwa
mwingine au kuambukiza mwingine ikiwa ni pamoja na VVU.
SABABU ZA KIBAIOLOJIA:
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 8 of 42
Wanawake ni rahisi kuambukizwa ugonjwa wa zinaa kutoka kwa mwanaume
aliyeathirika kuliko wanaume kutoka kwetu, kwa sababu vijidudu vya magonjwa
huweza kuingia kirahisi kwenye miili yetu. Na hatuwezi hata kujua kama tayari
tumeshaambukizwa. Vijidudu vinapokuwa tayari vimeshaingia ndani, hali ya joto
na unyevunyevu wa mwili huwa ni mazingira mazuri kwa hivyo vijidudu
kuendelea kukua na kuzaliana.
Mlango wa mji wa mimba kwa msichana mdogo huwa haujakomaa
mpaka anapofikisha umri wa kuanzia miaka kumi na nane - tisa, na hivyo huwa
kwenye hatari zaidi kupata uambukizo, na bado wengi wetu hujiingiza kwenye
vitendo vya ngono mapema zaidi kabla ya umri huo. Baada ya kukoma kwa
hedhi kwa mwanamke, kuta za ukeni huwa nyembamba sana na kuwa kavu
zaidi, kwa hiyo wanawake wenye umri mkubwa huweza kupata michubuko
midogo midogo kwenye ngozi wakati wa kujamiiana ambao huwa ni hatari kwa
maambukizo. Watoa huduma za afya mara nyingi huwa hawawapi ushauri
wanawake wenye umri mkubwa kuhusu kujikinga na kufanya vipimo. Kwa hiyo
tunaweza kudhani kuwa katika umri wetu hatari ni ndogo sana. Kama tutafanya
ngono na wanawake tu, uwezekano wetu wa kupata ugonjwa wa zinaa ni mdogo
sana, lakini pia wanawake huwaambukiza wanawake wengine magonjwa ya
zinaa. Wengi wetu ambao hujichukulia kama
SIDEBAR:
KUIJALI AFYA YAKO YA KIJINSIA.
1. Njia bora ya kuzuia kupata uambukizo wa ugonjwa wa zinaa ni kuepuka
kuambukizwa kwa mara ya kwanza. Wanawake wengi sasa hivi wanafikiri
kwamba kufanya ngono ni sehemu ya mategemeo ya kujenga uhusiano
mpya mara nyingi kabla ya kila mmoja kumfahamu vizuri mwenzake.
Katika umri wowote tunaweza kutaka kuchelewa kufanya ngono mpaka
tunapowafahamu vya kutosha wenzi wetu na kujadiliana kuhusu hatari ya
magonjwa na njia za kujikinga. Uhiari wa kuongelea ngono salama na
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 9 of 42
kinga dhidi ya ugonjwa wa zinaa inaweza kuwa ni kiashiria kizuri kama
kweli wenzi wote wako tayari kufanya ngono. Ni uamuzi wako. Watu
wengine hawana budi kuheshimu uchaguzi wako na hisia zako. Usikubali
kulazimishwa na mtu yeyote kufanya ngono kama hutaki.
2. Kama unataka kufanya ngono, uwe tayari kujikinga mwenyewe. Weka
tayari zana zako za kujikinga karibu na wewe. Kuwa nazo kabla hujaanza
kuchezeana, kwa sababu hisia zitakopokuwa kali unaweza kushindwa
kukatisha na kuzitafuta. (kwa maelezo zaidi, tazama sura ya 14, “ngono
salama”
3. Kama unaona ni vigumu kuzungumza na mwenzi wako kuhusu ngono
salama, unaweza kufanya mazoezi ya nini cha kusema na jinsi ya
kukizungumza na rafiki yako, au na mtoa ushauri nasaha katika kituo cha
afya au kliniki ya uzazi wa mpango.
4. Kama unafikiri kuna uwezekano wa wewe au mwenzi wako kupata
uambukizo, nenda kapime na upate matibabu haraka. Kumbuka
unaweza kuwa na ugonjwa wa zinaa bila ya kuonyesha dalili zozote.
5. Unaweza kufanyiwa vipimo hata kama hauonyeshi dalili zozote kwa
sababu baadhi ya magonjwa ya zinaa hayana dalili zinazoonekana. Ni
vizuri kufanya hivi kama ndio unaanza uhusiano mpya wa ngono, au kama
unafanya ngono na zaidi ya mtu mmoja, au kama unadhani au unafahamu
kuwa mwenzi wako ana mwenzi mwingine. Uliza ni magonjwa gani hasa
ya zinaa unayofanyiwa vipimo, baadhi ya magonjwa yanabidi yatambuliwe
kwa dalili kuonekana kwa sababu hakuna kipimo cha kuyatambua cha
kuaminika. Miongozo ya sasa hivi inapendekeza kuwa wanawake wenye
kufanya ngono wenye umri wa miaka ishirini na mitano na chini ya huu
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 10 of 42
umri kufanyiwa uchunguzi wa ugonjwa wa chlamydia kila mwaka, ambao
upo sana na unaweza kusababisha madhara makubwa kiafya kama
hautatibiwa.
6. Kama wewe au mwenzi wako mna ugonjwa wa zinaa ni hatari kufanya
ngono mpaka wewe na wenzi wako wa sasa hivi na wenzi wao pia
watakapokuwa wameshapimwa afya zao, kutibiwa na kupona. Muulize
mhudumu wa afya unatakiwa kusubiri kwa muda gani ili kuwa na uhakika
kwamba itakuwa salama kufanya ngono.
7. Kabla ya kukubali matibabu hakikisha unazifahamu dawa utakazozitumia
na ni kwa muda gani, na madhara yanayotokana na hizo dawa, na
kufuatilia vipimo vyovyote au matibabu. Usione aibu kuuliza maswali.
8. Muulize mhudumu wako wa afya kuhusu uwezekano wa kupata chanjo ya
ugonjwa wa manjano (Hepatitis B). .
9. Uchunguze mwili wako kila mara, hasahasa sehemu za siri, kuangalia
kama kuna tatizo lolote (tazama sura ya 13, -“viungo vya uzazi, na
mzunguko wa hedhi”). Unaweza kuhitaji kutumia spekilamu (kifaa cha
kupanulia viungo vya mwili ili kuona sehemu ambazo hazionekani kwa njia
ya kawaida) kuangalia ndani ya mlango wa kizazi. (kama unataka
kuagiza kifaa hiki, tazama “msaada”.) kama kuna kitu chochote
kinaonekana au kutoa harufu tofauti, unaweza kumuona mhudumu wako
wa afya ili akupime. Hata kama vidonda vikishapona, inaweza kuwa ni
dalili kuwa umeshapata uambukizo.
10 Fanya uchunguzi wa mara kwa mara kwenye eneo la nyonga, saratani
ya ukeni, na uchunguzi wa ugonjwa wa zinaa.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 11 of 42
11 Mtafute mtaalam wa afya ambaye utaweza kujadiliana naye kuhusu afya
ya uzazi. Mtafute mtu ambaye atakupa taarifa kamili na ya kueleweka,
mwenye kutia moyo na kujibu maswali, na kubali hali yako ya ujinsia.
Usimsubiri mshauri wako aanze kukuuliza maswali. Kama unahitaji
msaada, ulizia.
END SIDEBAR
Wengi wetu tunaojichukulia kama wasagaji tunaweza pia tukawa
tumeshafanya ngono na wanaume, hivi karibuni au zamani. Wakati huo
bado tuna hatari ya kupata uambukizo sawa kama wanawake wanafanya
ngono na wanaume.
Ni wapi tunaweza sasa kutofautisha kati ya “raha” na “kuwa salama”
haikubaliki? Hakuna kitu kinachoitwa ngono huria tena. Hii ni tofauti kabisa
na wakati wangu ni kikua.
MISINGI YA KIJAMII NA KIUTAMADUNI
Wanawake wenye umri wa miaka kumi na mitano mpaka ishirini na minne,
wenye mahusiano ya kingono na zaidi ya mwenzi mmoja au wanaoishi
maeneo ya mjini ambapo idadi ya watu wenye magonjwa ya zinaa ni kubwa
na uwezekano wa kupata maambukizi ni mkubwa basi wako katika hatari
kubwa sana ya kupata ugonjwa. Wengi wetu umaskini unachangia kwa kiasi
kikubwa zaidi kupata ugonjwa wa zinaa. Haimaanishi kwamba kutokuwa na
fedha za kutosha kutakuzuia kujikinga na kupata matibabu, utegemezi wa
kiuchumi kwa mwenzi ambaye anaweza kutuambukiza, au kubanwa na
pilikapilka za kimaisha za kila siku kuliko kitu kingine. Mambo mengine
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 12 of 42
tuliyopitia utotoni ikiwa ni pamoja na vurugu za kihisia na kijinsia, huongeza
hatari ya kupata ugonjwa wa zinaa baadaye maishani (tazama “Sura ya 8,
Vurugu na unyanyasaji”). Kama mila zetu zinadumisha kuwa mwanamke
anatakiwa kukubali na kutoonyesha hisia inaweza kuwa ni vigumu kukataa
kufanya ngono bila hiari na kujadili ngono salama. Kama utamaduni wetu
unatuzuia kugusa au kuangalia sehemu zetu za siri, hatutaweza kugundua
dalili za awali za ugonjwa wa zinaa.
MAGONJWA YA ZINAA NA UKEKETAJI
Wanawake waliokeketwa wako katika hatari kubwa zaidi ya kuambukizwa
ugonjwa wa zinaa kutoka kwa mwenzi aliyeathirika kwa sababu ya vidonda
visivyopona, uvimbe sehemu ya nje ya uke, au michubuko midogo midogo
inayotokana na kujamiiana. Wanawake ambao wameshonwa ukeni, au
wenye kovu kwenye mlango wa uke linalotokana na kukeketwa inakuwa ni
vigumu kwao kupona baada ya kuambukizwa hata kama watapata matibabu,
Kwa sababu maji maji ya ukeni hayawezi kutoka nje. Katika mazingira
mengine, kufanya upasuaji wa kufungua kovu hulazimika kufanyika kabla ya
uambukizo kupona kabisa. Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake au
kikundi cha kusaidiana ambacho huwasaidia kimwili na kihisia wanawake
waliokeketwa kinaweza kutoa ushauri zaidi kuhusu suala hili.
NIFANYE NINI KAMA NINAFIKIRI NIMEAMBUKIZWA UGONJWA WA
ZINAA?
Kafanyiwe uchunguzi mapema iwezekanavyo. Kama una umri wa chini ya
miaka kumi na minane, unaweza kufanyiwa uchunguzi na kutibiwa bila ya
idhini ya wazazi wako katika jimbo lolote.
SIDEBAR:
ZAWADI YA MAISHA YANGU:
JENIFFER BAUMGARDNER
Nilipokuwa na umri wa miaka ishirini na sita, niliambukizwa ugonjwa wa
malengelenge kutoka kwa kijana wa kiume anayevutia siku ya kwanza tu
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 13 of 42
tulipokutana. Hapo mwanzoni nilijipa moyo kwamba, maumivu niliyokuwa
nikiyapata ukeni, homa na fadhaa zilikuwa ni dalili mbaya za uambukizo
kwenye njia ya mkojo, lakini nilipokwenda kwa daktari wangu majibu
yalikuwa tofauti. Nilikuwa na HSV-1, kwa kawaida hufahamika kama
malenge lenge ya mdomoni, lakini mimi yalinitokea kwenye sehemu za
siri. Kwa sababu ya kufanya ngono ya mdomoni kumekuwa ni jambo la
kawaida, hivyo kupata huu uambukizo wa aina hii imekuwa ni jambo la
kawaida kupata malengelenge ya kwenye sehemu za siri.
Kusema kweli, hapo mwanzoni baada ya kufanyiwa uchunguzi na
kugundulika kuwa nina huu ugonjwa nilipata msongo wa mawazo sana.
Moja kwa moja nilienda kusoma kitabu changu cha afya cha Mayo na afya
ya miili yetu kwa siku kadhaa, nikitafakari maisha yangu ya baadaye
yatakuwaje. Kwa kweli vitabu vilinishitua kwa sababu vilielezea
uwezekano wa kupata madhara makubwa yatokanayo na malengelenge.
Kwa mfano, kila mwaka naweza kupata maambukizo, na inaonekana
kwamba ninaweza nikajifungua kwa upasuaji mkubwa kama nitapata
ujauzito. Kama kidonda kitasababisha uambukizo kwa mtoto wakati wa
kujifungua kwa njia ya kawaida, basi anaweza akapata upofu. Pia nilijihisi
nimeingia kwenye mtego wa uhusiano kwa mtu aliyeathirika ingawa
nilimpenda sana kwa sababu nilihofia kuwaambia wapenzi wengine au
kuogopa kutelekezwa. Hata hivyo ni miaka nane sasa sijapata tatizo lolote
na sasa hivi nina ujauzito wa miezi saba. Daktari wangu aliniambia
kwamba wanawake wengi huweza kujifungua kwa njia ya kawaida kama
tu ugonjwa haujajirudia rudia. Amenipa dawa(acyclovir) nizitumie ambazo
zitazuia kujirudia kwa ugonjwa katika mwezi wa mwisho wa kipindi cha
ujauzito wangu kama tahadhari.
Nilikuwa nimeshafanya ngono na wanaume watatu tangu yule mwenzi
kijana mzuri aliponipa zawadi yangu ya maisha. Taarifa ya ugonjwa
wangu ilipogundulika kwa wale wenzi wangu iliwauma sana – na mmoja
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 14 of 42
wao alikasirika sana baada ya kupata hii taarifa lakini haikuharibu maisha
yangu ya mapenzi. Niliendelea kuwa na uhusiano wa muda mrefu na yule
mwenzi ambaye alikuwa amekasirika sana, mwishowe hofu ilimwishia.
Kitu kibaya zaidi ambacho kilitokea ni kwamba nilimpa mtu mwingine ile
zawadi. Sikuwa na dalili lakini lazima nilikuwa na virusi na nilikuwa situmii
mipira ya kiume baada ya uhusiano kuendelea kukomaa. Ni kwa sababu
nilimwambukiza mwenzi mwingine.
Alipata uambukizo mkali mara moja na hakupata tena. Kitu kikubwa
kilichonipa moyo kupambana na uambukizo wa ugonjwa wa ngono ni kwa
vile nimekuwa mwanachama wa klabu kubwa: yenye watu milioni 40. Na
kitu kingine ambacho kilisaidia pia ni kumweleza baba yangu, kwa
kumwelezea Baba yangu ambaye ni daktari katika mji wetu wa Fargo, ND.
Kitu cha kwanza alisema halitakuwa ni tatizo kubwa. Malengelenge ni
moja kati ya magonjwa yenye madhara madogo utakayoyapata.” Alikuwa
sahihi.
WAPI PA KWENDA KUPATA HUDUMA:
• Kliniki za afya za umma. Kliniki za magonjwa yanayoambukizwa kwa njia
ya ngono zilizo chini ya udhamini wa serikali hutoa huduma bure kwa
vijana na hutoa pia huduma bila kujali uwezo wa mtu wa kulipa.
Wataalamu wa kliniki za magonjwa ya zinaa ni wenye ujuzi wa hali ya juu
katika kufanya vipimo, kufanya uchunguzi, na kutibu magonjwa ya aina hii,
na mazingira ya matibabu huwa ni ya usiri zaidi kuliko ya ofisi ya
wahudumu wa kawaida. Ili kupata huduma kwenye kituo cha karibu
wasiliana na vituo vya taifa vya kudhibiti magonjwa ya zinaa kupitia
namba hii ya simu 1-800-227-8922.
• Kliniki za uzazi wa mpango:
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 15 of 42
Wataalam wengi wa uzazi wa mpango pia hutoa ushauri nasaha kuhusu
magonjwa ya ngono na upimaji au rufaa. Na hata kama hawatoi huduma hizi
watakuelekeza wapi utakapozipata. Pia hutibu kwa umakini na adabu. Wengi
wao huduma zao huwa ni za gharama nafuu na huduma hutolewa kutokana na
kipato cha mtu.
• Wataalam wa afya ya jamii (madaktari). Nenda kwa wahudumu wako wa afya
wa siku zote kama utajisikia huru kuongea nao na kama wanatoa majibu
mazuri yanayoeleweka ya maswali yako. Licha ya hivyo, sio wataalam wote
wana vifaa vya kufanyia vipimo vya ugonjwa wa zinaa kila mara, na pia
wanaweza kuwa hawafahamu kwa undani zaidi kuhusu haya magonjwa.
Unaweza kutaka kuuliza kama matibabu yako yanafuata miongozo ya vituo vya
sasa vya udhibiti wa matibabu ya magonjwa, ambayo inapatikana kwenye
mtandao (tazama, www.cdc.gov/std/treatment/).
• CHUMBA CHA DHARURA:
Hapa siyo mahali pazuri pa kwenda, kwa sababu kwenye chumba cha
dharura cha hospitali hutapata muda wa kuongea na daktari, tiba ya
kitaalam, na ya umakini ambayo unaihitaji ili kupambana na masuala
yanayohusu magonjwa ya ngono, isipokuwa kama unahitaji huduma ya
dharura. Au kama ulilazimishwa kufanya ngono na una wasiwasi kwamba
utakuwa umeambukizwa ugonjwa wa zinaa, vyumba vyote vya dharura
vinaweza kukupa matibabu ya kinga kwa ajili ya magonjwa ya ngono,
pamoja na VVU.
JIANDAE KWENDA KUPATA HUDUMA YA AFYA.
• Wasiliana nao kwanza ili kujua ni huduma gani zinazotolewa na kiasi gani
utatakiwa kulipa. Mara nyingi vipimo hufanywa bure, lakini kunaweza kuwa na
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 16 of 42
gharama ya kumwona daktari. Kama hutaki wazazi wako wafahamishwe au
kupelekewa gharama za matibabu au ujumbe, muulize mhudumu wako kuhusu
utaratibu wao. Muulize kuhusu utaratibu wa kulipia gharama za matibabu (bili)
unakuwaje, na muulize kama anafahamu jinsi mpango wa matibabu yako
unavyoenda.
• Muone daktari haraka, hata kama dalili hazikuletei maaumivu. Magonjwa
mengi ya ngono yanaweza kuchunguzwa kwa usahihi zaidi kama tayari una
dalili zake. Wahudumu mara nyingi wanaweza kuchunguza ugonjwa wa
malengelenge kwa kuangalia kwa macho ila vipimo vya maabara huwa sahihi
zaidi kwa kutumia sampuli kutoka kwenye vidonda. Kipimo cha damu cha
kutofautisha aina ya I na ya II ya ugonjwa wa malengelenge sasa hivi
kinapatikana.
• Jaribu kujipatia huduma ya kwanza wakati unasubiri kwenda kumwona
daktari, ila usiweke krimu yoyote au mafuta kwenye kidonda kisichokuwa na
maumivu kwa sababu zinaweza kuwaharibu bakteria na kufanya vipimo visitoe
majibu sahihi.
• Usifanye ngono au kusafisha ukeni kabla hujaonana na daktari. Kwani
vitendo hivi pia vinaweza kufanya majibu yasiwe sahihi na kuharibu uchunguzi.
KUPATA HUDUMA NA MATIBABU
Popote unapokwenda kwa ajili ya kupata huduma una haki ya kupatiwa matibabu
yanayostahili na kwa adabu. Ni wazo zuri kusindikizwa na mtu ili aandike
maelezo ya daktari na kukufariji kihisia.
• Uwe tayari kutoa historia kamili ya afya yako na kufanyiwa uchunguzi kwenye
sehemu zako za siri (tazama sura ya 28, “pekee kwa wanawake”).
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 17 of 42
• Muombe mhudumu wa afya akuelezee vipimo vyovyote, utakavyofanyiwa
matibabu na madhara yake kwa njia ambayo unaweza kuifuata. Hakikisha
unaelewa chaguzi zako zote za matibabu.
• Kabla hujaondoka, hakikisha kwa njia utakayoelewa. Hakikisha unelewa
utaratibu wa matibabu yako na maamuzi uliyoyafanya.
• Kabla ya kuondoka, uelezwe lini utarudi kwa ufuatiliaji. Kama daktari wako
hana muda wa kujibu maswali, omba kuongea na mtu mwingine.
Usiondoke kabla ya maswali yako kujibiwa. Muulize itachukua muda gani
kwa hizo dalili kuisha kabisa. Na kama hazitaisha, rudi tena kwa
uchunguzi mwingine.
• Kama una maswali zaidi baada ya kutoka kwa daktari, piga simu na
uulizie taarifa unazozihitaji.
• Tumia dawa yote ya ugonjwa wa ngono hata kama umepata nafuu au
kama dalili zimeisha. Usichangie dawa yako na mtu mwingine. Kila mtu
anatakiwa awe na matibabu yake mwenyewe.
• Wewe na wenzi wako (na wenzi wao) lazima mtibiwe na kutumia dawa
zote kama ilivyoelekezwa na daktari kabla ya kufanya ngono tena. Kama
mtakiuka hayo maagizo mtaendelea kuambukizana. Subiri mpaka
utakapomaliza dawa au daktari wako atakapokupa idhini.
• Kama unapata maumivu wakati wa kukojoa acha kunywa pombe mpaka pale
uambukizo utakapoisha kabisa. Pombe inaweza kusabaisha mwasho kwenye
njia ya mkojo.
Unaweza pia usipate nafuu baada ya kupata matibabu hayo. Wakati mwingine
vipimo huwa sio sahihi; na wakati mwingine matibabu huwa ni mzigo au
hayasaidii na hii inamaanisha kwamba utazidi kwenda kumwona daktari ukitumia
muda mwingi na fedha. Lakini njia mbadala ya kutopata matibabu ni hatari zaidi.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 18 of 42
VIKWAZO VYA KUKABILIANA
Ubaguzi wa aina yoyote kwenye mfumo wa matibabu unafanya iwe ni vigumu
kujadili kuhusu masuala ya ngono, hatari ya magonjwa ya ngono na maambukizi.
Wataalam wengi wa afya bado wana mtazamo hasi dhidi ya ujinsia wa
wanawake. Wengine huwa na ubaguzi wa kimbari au kuchukia uhusiano wa
jinsia moja. Huwa na dhana kwa wanawake weusi na wenye vipato vidogo, lakini
hawathubutu kuwajaribu wanawake wa kizungu, wa tabaka la kati, au
mwanamke mwenye umri mkubwa zaidi, au mwanamke mzuri aliyeolewa hata
kama ana dalili za ugonjwa.
Mara ya kwanza nilipomwomba daktari wa magonjwa ya wanawake kuwa nina
taka kufanyiwa kipimo cha kaswende, alitoa tabasamu na kuniangalia kwa kejeli
na kusema “Nina hakika kuwa hakuna mwanaume uliyetembea naye kuwa na
kaswende”
Ilianza kama uvimbe uliojaa maji. Miezi michache baadaye nilianza kuhisi homa,
mfadhaiko, na maumivu makali chini ya tumbo (kwenye fumbatio)…Baada ya
miezi tisa niligundulika kuwa nilikuwa na ugonjwa kwenye via vya uzazi (PID)
ambao wanauita “ni uambukizo mdogo tu wa via vya uzazi”. Mpaka pale mume
wangu alipoonyesha dalili ndipo walipokuwa makini kwangu na kututibu wote
pamoja na mume wangu kwa dawa sahihi.
Kwa wasagaji kujitambulisha kwa mtaalam wa afya lazima uhakikishe unapata
taarifa sahihi, vipimo, na matibabu kwa ajili ya dalili za ugonjwa wa zinaa. Licha
ya hivyo, hata kama tukielezea mienendo yetu ya kingono baadhi ya wataalam
bado hawajapata mafunzo ya kuelewa matakwa ya wanawake ambao
wanafanya ngono na wanawake wenzao.
Hivi karibuni, nilienda kwa daktari mwanamke bingwa wa wanawake, na
nikamwambia kuwa nilikuwa nafanya ngono na wanawake…baadaye, wakati
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 19 of 42
akinifanyia uchunguzi alisema hakukukuwa na haja ya kupima magonjwa ya
ngono. Nilishangazwa sana. Alifikiri kwamba siwezi kuambukizwa magonjwa ya
ngono kwa sababu wenzi wangu ni wanawake. Kwa bahati nzuri, nilijua kwamba
hakuwa sahihi…
Jaribu kumtafuta daktari mwenye uzoefu wa kutosha au muuguzi ambaye
unaweza kuongea naye kwa uhuru kuhusu afya yako ya ngono kabla hujapata
matatizo yoyote. Halafu utajua wapi pa kwenda kwa ajili ya huduma kama
utahitaji.
MAGONJWA YA ZINAA NA SHERIA
Madaktari na vituo vya kutolea huduma kwa mujibu wa sheria wanatakiwa kutoa
taarifa kuhusu maambukizi yote ya kisonono na kaswende, pamoja na UKIMWI
kwa serikali au afisa wa afya wa karibu.
Chlamydia na chancroid (magonjwa yanayoambukizwa na bakteria yenye
vidonda vyenye maumivu makali) yanatolewa taarifa katika majimbo mengi. Pia
taarifa ya maambukizi ya VVU inatolewa katika majimbo mengi. Granuloma
inguinale (uvimbe sugu kwenye sehemu za siri) na lymphogranuloma
venereum (ambao husabishwa na aina nyingine ya chlamydia), mara nyingi
huwa katika nchi zenye hali ya joto na zenye joto kidogo pia huripotiwa kwenye
majimbo mengi.
Kama una kisonono au kaswende mtoa huduma wa afya anaweza
kukuuliza majina ya watu uliofanya nao ngono (inawezekana walikuambukiza au
umewaambukiza haya magonjwa). Inabidi wafahamishwe bila ya jina lako
kutajwa ili kulinda usiri wako. Kama hutaki kutaja majina yao waambie
utawasiliana nao wewe mwenyewe. Kwa hiyo ni jukumu lako kuwasiliana na kila
mtu ambaye ulifanya naye ngono na kumwambia aende akapatiwe matibabu.
Kwa kufanya hivyo kutawanusuru kutopata utasa na hata kuokoa maisha yao na
ya wenzi wao wa baadaye.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 20 of 42
Pia una haki ya kupatiwa matibabu na kuhifadhi taarifa za ugonjwa wako kwa
usiri bila ya mtu mwingine kujua (tazama Sura ya 30, “Kuongoza mfumo wa
huduma ya afya”).
UJAUZITO NA MAGONJWA YA ZINAA.
Magonjwa ya zinaa hupunguza au huhatarisha uwezo wetu wa kupata ujauzito
na kuleta matatizo wakati wa ujauzito. Na pia huweza kumuathiri kiumbe aliye
tumboni au mtoto atakayezaliwa.
VIPIMO VYA KUFANYA KABLA YA KUJIFUNGUA
Kufanyiwa vipimo kabla ya kuonyesha dalili ili kuangalia kama kuna ugonjwa
wowote ni muhimu. Wanawake wote wajawazito wanatakiwa wafanyiwe vipimo
vya VVU na kupimwa kisonono, homa ya manjano B, chlamydia na kaswende.
Kipimo cha homa ya manjano C kimependekezwa kwa wanawake wanaotumia
dawa za kulevya zinazochomwa kwenye mishipa ya damu au waliopewa
virutubisho vya damu, au kuongezewa damu, au waliopandikiziwa viungo.
Kuanza kliniki mapema wakati wa ujauzito ni wakati mzuri wa kupima
uambukizo wa Bakteria wa ukeni (BV) na kufanyiwa kipimo cha saratani ya ukeni
kama hakikufanywa mwaka uliopita.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 21 of 42
MGONJWA MAKUU YA NGONO YANAYOSABABISHWA NA BAKTERIA
(Yanaweza kutibika kama yatagundulika mapema na kutibiwa kwa kiua vijasumu)
KISABABISHO UNAVYOENEZWA DALILI ZINAZOONEKANA DALILI ZA
KAWAIDA
VIPIMO /NA TIBA MADHARA YAKE
CHLAMYDIA
Ngono ya ukeni,
mdomoni (na mara
chache), kupitia njia
ya haja kubwa
Kushika macho kwa
mikono yenye maji
maji yenye
uambukizo.
Kutoka kwa Mama
kwenda kwa mtotowakati
wa kujifungua.
Uvimbe kwenye via vya
uzazi. Muda haujulikani
Dalili zingine kuanzia siku
7-14.
Wanawake: hakuna
dalili kwa
wanawake 4 kati ya
5. Kama mlango
wa kizazi
umeathirika, uchafu
hutoka ukeni, kuhisi
maumivu wakati wa
kukojoa, kutokwa
damu ukeni kusiko
kawaida, kutokwa
na damu baada ya
kufanya ngono.
Kama ni uvimbe wa
Wanawake: uchunguzi
wa sampuli ya
fupanyonga; kipimo cha
mkojo.
Wanaume: sampuli ya
njia ya mkojo, kipimo cha
mkojo.
Vinaweza
vikawatatanisha na
kisonono. Fanyiwa
vipimo vya haya
magonjwa yote.
Tiba: Vidonge.
Wanawake:
Uvimbe wa via vya
uzazi unaweza
kusababisha
maumivu sugu ya
nyonga, utasa,
matatizo ya
ujauzito (utungaji
wa mimba nje ya
kizazi).
Wanaume: Uvimbe
kwenye mirija ya
mbegu za uzazi,
Korodani na tezi
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 22 of 42
fupanyonga (PID):
kutokwa damu na
maumivu chini ya
tumbo. Mlango wa
kizazi huonekana
kuvimba. Uvimbe
kwenye njia ya haja
kubwa (proctitis)
Wanaume: uume
kuwaka moto,
kutokwa na uchafu
kwenye uume.
Kunaweza
kusababisha
uvimbe kwenye njia
ya mkojo.
(urethritis).
kibofu.
Watoto wachanga:
Hupata uambukizo
wakati wa kuzaliwa,
kupata uambukizo
kwenye macho na
nyumonia.
KISONONO Kufanya ngono ya
ukeni, mdomoni na
Kutoka siku 2-30 (wastani
siku 3 -7)
Wanawake: Wengi
hawaonyeshi dalili.
Wanawake: sampuli ya
uchunguzi wa
Wanawake:
Uvimbe wa via vya
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 23 of 42
kupitia njia ya haja
kubwa.
Kushika macho kwa
mikono yenye
majimaji yenye
uambukizo.
Kutoka kwa mama
kwenda kwa mtoto
wakati wa kujifungua.
Kama mlango wa
kizazi umeathirika,
hutokwa na usaha
mzito au damu
ukeni; vidonda
kwenye koo,
maumivu makali
wakati wa kukojoa,
kutokwa na mitoki
(karibu na sehemu
za siri) maumivu ya
rekta au uvimbe
(proctitis), kutokwa
na uchafu kwenye
njia ya haja kubwa,
kuathirika macho
ambapo
husababisha upofu
kwa watu wazima
na watoto
wachanga.
fupanyonga; kipimo cha
mkojo.
Wanaume: sampuli ya
njia ya mkojo na ; na
kipimo cha mkojo.
Vinaweza kuwatatanisha
na ugonjwa wa
chlamydia kwa hiyo
fanyiwa vipimo vya haya
magonjwa yote.
Tiba: vidonge au
sindano.
uzazi (tazama
hapo juu)
Wanaume:
Kuvimba kwa
korodani, tezi
kibofu ; utasa
(hutokea kwa
nadra)
Wanawake na
wanaume: kama
hawakutibiwa,
maambukizo
huenea, (ni nadra
lakini huwa na
madhara
makubwa) wakati
bakteria
wanaposafiri kupitia
mishipa ya damu;
husababisha
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 24 of 42
Wanaume:
kutokwa na usaha
mzito kwenye
uume; uume
kuwaka moto
wakati wa kukojoa.
Dalili zingine
zinafanana na za
wanawake
(vidonda vya koo,
maumivu ya
kwenye rekta au
kutokwa na uchafu,
kuathirika macho)
harara kwenye
ngozi, uvimbe
wenye maumivu
kwenye maungo ya
mwili ; kuathirika
kwa valvu za
kwenye moyo
(nadra), ugonjwa
wa baridi au homa
ya uti wa mgongo.
Mtoto mchanga :
Huweza
kumuambukiza
mtoto anayezaliwa,
na kumsababishia
kupata upofu kama
hatapata kinga
wakati wa kuzaliwa.
KASWENDE Kufanya ngono/
kugusana ngozi na
Hatua ya kwanza:
Siku 10 -90 (wastani wiki 3
Wanawake na
wanaume, hatua ya
Kupima damu; tiba:
sindano
Wanawake na
wanaume: kama
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 25 of 42
mtu aliyeathirika.
Huambukiza kupitia
vidonda vilivyo wazi
au vipele sehemu
yoyote kwenye mwili.
Unaweza
kumuambukiza mtoto
kabla ya kujifungua.
Hauwezi kuambukiza
baada ya miaka
michache ya hatua
ya fiche.
Hatua ya pili: mwezi 1-6. mwanzo: vidonda
visivyokuwa na
maumivu kwenye
uke au kuzunguka
uke (kwenye
mashavu au ndani),
kwenye uume,
mdomo, na njia ya
haja kubwa;
kwenye mwili
popote vijidudu vya
bakteria
vitakapoingia
(kwenye ncha za
vidole, midomo au
matiti). Vidonda
hupona ndani ya
wiki 1-5, lakini
bakteria huendelea
kubaki mwilini.
Hatua ya pili.
hawatapatiwa
matibabu: hupata
upofu, huathiri
ubongo, magonjwa
ya moyo, ulemavu,
ugonjwa wa baridi,
kupooza kwa mwili.
Mtoto mchanga:
huathiri mifupa ya
mtoto, macho,
ngozi, meno na ini
wakati wa
kujifungua. Wakati
mwingine hupoteza
maisha.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 26 of 42
Kutokwa na vipele
au chunusi
zisizowasha usoni,
mwilini, kwenye
viganja vya mikono,
unyayo; kuwa na
dalili za mafua,
kutokwa na matezi,
kunyonyoka
nywele, kutokwa na
malengelenge.
Dalili zote za hatua
ya pili huisha kwa
matibabu kama
baada ya mwezi
mmoja.
Dalili fiche: hubaki
mpaka baada ya
miaka 20 bila ya
dalili zozote
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 27 of 42
kuonekana;
vijidudu vya
bakteria vinaweza
kushambulia ndani
ya ogani, ikiwa ni
pamoja na moyo na
ubongo.
Hatua ya tatu:
tazama madhara
yake.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 28 of 42
MAGONJWA MAKUU YA NGONO YANAYOSABABISHWA NA VIRUSI
(Hayatibikii lakini tiba inapatikana)
KISABABISHO JINSI
UNAVYOAMBUKIZA
DALILI
ZINAZOONEKANA
DALILI ZA
KAWAIDA
VIPIMO NA MATIBABU MADHARA YAKE
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 29 of 42
Malengelenge
aina ya I na II
Aina ya I mara
nyingi hutokea
mdomoni; licha
ya hivyo aina
zote mbili ya I na
II huweza pia
kuathiri kwenye
njia ya viungo
vya uzazi
Aina ya Pili,
hujulikana kama
malengelenge
ya viungo vya
uzazi, na ni
hatari zaidi.
Kufanya ngono
Huambukiza wakati
muathirika hajaanza
kuonyesha dalili na
wala hajui kama
ana virusi.
Virusi hujazana eneo
hilo ambalo
uambukizo ulianzia.
Dalili za Mwanzo:
mara nyingi siku ya
2-10; dalili
zinaweza kurudia
rudia kuonekana,
mara nyingi katika
miezi ya 3-12.
Hakuna hata
mmoja kati ya watu
wote
walioambukizwa.
Kishada cha
vidonda vyenye
maumivu makali
sana kwenye eneo
la viungo vya uzazi.
Maumivu wakati wa
kukojoa, kutokwa
na uchafu, kutokwa
na mitoki, homa,
maumivu ya mwili.
Mara nyingi dalili
hurudia rudia
kutokea katika
mahali ambapo
virusi waliingia kwa
mara ya kwanza
kwenye mwili.
Hutokea zaidi
kama katika hatua
ya mwanzo
madhara yalikuwa
makubwa na
yalisababishwa na
ugonjwa huu aina
ya II. Hatua
zinazojirudia mara
nyingi hazina
madhara
makubwa; na
huchochewa na
shinikizo au
Uchunguzi wa kuangalia
kwa macho na
uchunguzi wa sampuli
za majimaji ya
malengelelenge
unaofanywa maabara.
Vipimo vipya vya damu
vinaweza kugundua aina
ya I na aina ya II.
Dawa za kinga dhidi ya
hivi virusi (vidonge)
huweza kupunguza dalili
na kushambuliwa mara
kwa mara.
Mtu anaweza kuishi
maisha yake yote na
uambukizo huu.
Dalili hutofautiana kwa
kila mtu. Huweza
kusababisha mfadhaiko
wa kihisia na kimwili pia.
Pamoja na kusindwa
kutoa haja ndogo, lakini
watu wengi hukabiliana
vizuri na hiyo hali. Vikundi
vya msaada vinapatikana.
Huweza kumuambukiza
mtoto wakati wa
kujifungua (huzidiwa
sana). Wengi huweza
kuwaambukiza watoto
wachanga kama mama
alipata uambukizo karibu
na wakati wa kuifungua.
Ni asilimia moja tu ya
wanawake wanao rudiwa
rudiwa na haya magonjwa
huwaambukiza watoto
wao. Ili kuepuka
kumuambukiza mtoto
mama hujifungua kwa
upasuaji mkubwa ili mtoto
asigusane na
malengelenge ya kwenye
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 30 of 42
kupungua kwa
mvutano. Ila kwa
baadhi ya watu
dalili kamwe
haziwarudii.
uke.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 31 of 42
KISABABISHO UNAVYOENEZWA DALILI ZINAZO
ONEKANA
DALILI ZA
KAWAIDA
VIPIMO / TIBA MADHARA YAKE
Virusi vya
Human (HPV)
Papiloma viko
vya aina 100,
lakini aina 30
huambukizwa
kwa njia ya
ngono.
Viotea sehemu
za siri (Ni aina
ya ugonjwa wa
ngono
unaosababishwa
na virusi vya
papiloma)
Kufanya ngono na
mtu mwenye
uambukizo.
Kugusana na viotea
(ndani ya uke).
Viotea
vikishaondolewa,
virusi vinaweza
kuendelea kuwepo
kwenye eneo la asili
la uambukizo.
Huchukua miezi
kadhaa hadi miaka
kuonyesha vidonda
kwenye mlango wa
kizazi.
Wiki 3 – hadi miezi
kadhaa kuonekana
viotea.
Virusi –
Havionekani;
Vidonda vidogo
visivyokuwa na
maumivu kwenye
mlango wa kizazi.
Uongezekaji wa
Viotea, wakati
mwingine huwa na
maumivu,
huwasha, hutoa
damu. Viotea
hukua kipindi cha
ujauzito, huwa
kama kabichi kadiri
vinavyozidi kuwa
vikubwa zaidi.
Kuzunguka njia ya
haja kubwa
kunaweza kutokea
uvimbe kimakosa.
Viotea hurudi tena
baada ya matibabu.
Virusi vya
Papiloma: Kipimo
cha saratani ya
mlango wa kizazi
kila mwaka
kuangalia seli
zozote ambazo
zimeathirika
kwenye mlango
wa kizazi. Kifaa
cha kuchunguza
uambukizo ukeni
(uchunguzi usio
na maumivu
unaotumia lenzi ili
kukuza) ili
kuthibitisha
kuwepo kwa seli
zisizo za
kawaida.
Uondoaji wa
sampuli za tishu
(sampuli ndogo
za seli) pima
vidonda ili kubaini
kuwepo kwa
saratani ya
mlango wa kizazi.
Aina nyingine za virusi
vya Papiloma
huongeza hatari ya
saratani ya mlango wa
kizazi (aina tofauti
husababisha uvimbe)
Uvimbe: huweza
kuziba njia ya uke,
uume na rekta.
Wakati wa ujauzito
uvimbe ndani ya uke
huweza kuwa mkubwa
zaidi, na kufanya ruta
za uke kutovutika
sana na kuleta
matatizo wakati wa
kujifungua. Wanawake
wengine wameripotiwa
kutofurahia tendo la
ngono kwenye
sehemu iliyoathirika
hata baada ya uvimbe
kutolewa.
Huweza kuathiri koo la
mtoto wa kati wa
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 32 of 42
Uvimbe:
huchunguzwa
kwa kuangalia.
Uvimbe huweza
kuondolewa kwa
myeyusho wa
topical,
kugandisha,
upasuaji na leza.
kujifungua (kwa
nadra)
Ugonjwa wa
manjano- B
(hepatitis B)
Kufanya ngono na
kuchangia sindano,
huweza
kumuambukiza mtoto
kabla na baada ya
kujifungua.
Wiki 6 – miezi 6 Kukosa hamu ya
kula, kuwa
mdhaifu, maumivu
ya misuli, kuumwa
kichwa, homa,
mkojo wenye rangi
nyeusi, dalili
zinaweza kuwa sio
rahisi kuzigundua.
Kipimo cha damu Baadhi ya watu
waliombukizwa
huweza kuwa
wasambazaji sugu.
Huweza kusababisha
matatizo sugu ya ini,
na saratani ya ini.
Virusi vya
Ukimwi (VVU).
(Tazama sura ya
16, “VVU na
UKIMWI”
Kufanya ngono na
mtu aliyeathirika
(damu, majimaji ya
mwilini); kuchangia
sindano;
kunyonyesha maziwa
ya mama; huweza
Kupima damu
kuangalia uambukizo
wa VVU; mara nyingi
uambukizo
huonekana baada ya
wiki sita au miezi
mitatu.
Mara nyingi hakuna
dalili au dalili
zinaweza kuwa
kidogo. Dalili huwa
ni pamoja na
kutokwa na mitoki,
vidonda vya koo.
Vipimo vya damu;
wanawake
wajawazito
hupimwa na
kupatiwa
matibabu ili
kuzuia
Virusi
vinavyosababisha
UKIMWI; nyumonia na
maambukizi mengine;
Kaposi’s sarcoma
(Uvimbe)
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 33 of 42
kumuambukiza mtoto
kabla na baada ya
kujifungua
Kuongezwa damu,
kushika majimaji
yenye virusi.
Kuchangia sindano.
Kunyonyesha mama
akiwa mwathirika.
Baada/ kabla ya
kuzaliwa.
Inaweza kuchukua
miaka kumi au zaidi
kwa UKIMWI kuanza
kuonyesha dalili.
Pia, kutokwa na
jasho usiku,
kupungua uzito, na
kutokwa na
vidonda mdomoni.
kumuambukiza
mtoto.
Tiba yake ni
ngumu
Mtoto anaweza kupata
uambukizo lakini kuna
dawa za kuzuia mara
nyingi kwa wanawake
wenye VVU. Dawa
zingine za UKIMWI
zina madhara
makubwa
MAGONJWA MENGINE
KISABABISHO UNAVYOENEA DALILI
ZINAZOJITOKEZA
DALILI ZA
KAWAIDA
VIPIMO / TIBA MADHARA YAKE
Trichomonsas
vaginalis
(Majimaji ya
ukeni yenye
harufu)
Kwa kufanya
ngono. Kugusana
na majimaji
baada ya kufanya
ngono (vijidudu
hivi huweza
kuishi kwenye
Ndani ya miezi 6
au mapema zaidi.
Wanawake :
kutokwa na
mapovu, uchafu
wenye harufu
mbaya wenye
rangi ya kijani na
njano, kuwashwa
Kufanyiwa uchunguzi
uchafu unaotoka
uumeni/Ukeni kwa
hadubini, na
kuotesha hizo
sampuli maabara.
Husababisha matatizo
kwenye ujauzito (endapo tu
utakuwa umeambukizwa
kipindi cha ujauzito).
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 34 of 42
mazingira ya joto,
unyevunyevu, nje
ya mwili)
ukeni, au kuwa
wa rangi
nyekundu. Pia
kuhisi maumivu
makali wakati wa
kujamiiana,
kutojisikia vizuri
chini ya tumbo na
kupata maumivu
wakati wa
kukojoa.
Wanaume: Mara
nyingi
hawaonyeshi
dalili. Wakati
mwingine
kutokwa na
usaha; kukojoa
mara kwa mara
na kuhisi
maumivu makali.
Tiba: vidonge: lazima
kuacha pombe
Bacteria
vaginosis,
Candida,
Monilia ( Aina
ya fangas)
Huambukizwa
kwa ngono au
bila kufanya
ngono, pamoja
na wanawake.
Endapo mabadiliko
ya kiwango cha pH
na bakteria wasio
hatari (flora) wa
ukeni
yanayosababishwa
na mabadiliko
yanayotokea kabla
ya siku za hedhi,
Uambukizo wa
bakteria ukeni
(BV) mpaka
asilimia 50 ya
wanawake
hawajaonyesha
dalili. Na dalili
zake ni kutokwa
na uchafu ukeni,
Uchunguzi wa
sampuli ya uchafu
wa ukeni kwa
hadubini, kipimo cha
pH, harufu ya uchafu
wakati wa kupima.
Vidonge au dawa za
krimu za kupaka
Vijidudu wa Bakteria ukeni
wakati wa ujauzito
husababisha kutoka kwa
mimba, kupasuka kwa
chupa mapema, kusikia
uchungu kabla ya muda, na
kujifungua kabla ya muda
unaotakiwa, na kutoka kwa
kizazi baada ya kujifungua.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”). For more information, see:
http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 35 of 42
mzunguko wa
hedhi, uzazi wa
mpango,
kujamiiana, kupiga
bomba au dawa
nyingine zenye
kemikali, kiua
vijasumu, na
mambukizo
mengine.
wenye harufu
mbaya. Pamoja
na mwasho lakini
sio wakati wote.
Fangasi: kutokwa
na uchafu mwingi
“wenye utelezi”
na harufu kidogo.
Mara nyingi
huwasha. Mara
nyingine uke
huwa mwekundu,
huvimba, harufu
huzidi kuwa
mbaya baada ya
kufanya ngono.
ukeni.
Ugonjwa huu huweza
kusababisha kuvimba kwa
fupanyonga au uambukizo
baada ya kufanyiwa
operesheni. Matibabu ya
kuzuia uambukizo huweza
kuwanufaisha wanawake
wenye dalili na wasio kuwa
nazo wakati wa ujauzito na
wakati wa kutoa mimba na
upasuaji wa kuondoa
mfuko wa kizazi.
Ugonjwa wa
ngozi – upele
unaowasha na
kutoa vidondachawa
na
viroboto.
Kufanya ngono
na kugusana kwa
mwili kwa namna
nyingine. Wakati
mwingine kupitia
kwenye nguo au
kuchangia
kitanda.
Wiki 2-4 Kuwashwa sana,
utitiri unaotembea
chini ya ngozi. Na
chawa kutaga
mayai kwenye
nywele.
Kufanya uchunguzi
kwa kuangalia
sampuli ya ngozi.
Dawa za kupaka
kwenye ngozi.
Kujikuna na kujichubua
kunaweza kusababisha
uambukizo.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 36 of 42
Unaweza ukapata uambukizo mpya wa ugonjwa wa zinaa. Uambukizo
unaoupata wakati wa ujauzito mara nyingi huenda hadi kwa mtoto aliye tumboni.
Utatakiwa ufanyiwe vipimo zaidi kama utakuwa kwenye hatari ya kupata
maambukizo wakati wa ujauzito wako. Pia, endelea kutumia mpira wa kiume na
kinga nyingine ili kujilinda dhidi ya uambukizo mwingine.
KASWENDE NA UJAUZITO
Mwanamke mjamzito aliye na kaswende anaweza kumuambukiza mtoto
aliye tumboni hasa katika miaka ya mwanzo ya uambukizo. Kama matibabu
yatafanyika mapema wakati wa ujauzito, mtoto anaweza asiambukizwe. Kama
matibabu yata fanyika baadaye sana wakati wa ujauzito, dawa itazuia ugonjwa
kuendelea lakini haitaweza kurekebisha uharibifu uliyokwisha tokea kwa mtoto
ambaye hajazaliwa (mtoto anaweza kufia tumboni au kuwa na hitilafu mbaya
atakapozaliwa). Kila mwanamke anatakiwa apime kipimo cha kaswende mara
anapotambua kuwa ni mjamzito, kabla ya kujifungua, na wakati wowote ambao
anadhani kuwa na uwezekano wa kupata uambukizo.
MALENGELENGE NA UJAUZITO
Malengelenge ni uambukizo hatari sana kwa mtoto anayezaliwa. Wanawake
wajawazito ambao hawana huu ugonjwa hawana budi kuepuka kufanya ngono
isiyo salama na wenzi ambao tayari wana huu uambukizo. Mwambie mtaalam
wako wa afya kama una dalili za ugonjwa wa malengelenge. Kama
umeshaonyesha dalili za huu ugonjwa au madhara yameshakuwa makubwa na
kusababisha vidonda wakati wa kujifungua unaweza ukafanyiwa upasuaji
mkubwa. Baada ya kujifungua, kuwa mwangalifu ili usimwambukize mtoto.
Usiviguse vidonda, na hakikisha umeosha mikono yako vizuri kabla ya kumshika
mtoto.
KUISHI NA UGONJWA WA MALENGELENGE.
Watu wengi hupata dalili za awali ambazo huashiria kuwa mtu
ameshaambukizwa: kama kuwakawaka moto sehemu hiyo uliyopata
uambukizo, kuwashwa, maumivu, kuhisi kuungua, au kuvuta hasa sehemu
iliyoathirika, na baadaye vidonda hutokea, huanza kama uvimbe mwekundu na
kubadilika kuwa malengelenge yenye maji ndani ya siku moja au mbili. Baada ya
siku chache, ukurutu hutokea na vidonda hupona. Wanawake walioathirika
vibaya sana wanaweza kushindwa hata kukojoa. Wasiliana na mtaalam wako wa
afya wa karibu kama hali hii ikitokea. Dalili zinazotokea mwanzoni mara nyingi
huwa na maumivu makali sana na huchukua muda mrefu kupona.
Inakuwa ni vigumu kukubali kuishi na huu ugonjwa wa malengelenge moja kwa
moja kama sehemu ya maisha. Unaweza kupata mshituko utakapogundua kuwa
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 37 of 42
umeambukizwa ugonjwa wa malengelenge na hauwezi kupona. Unaweza kujihisi
kutengwa, mpweke, na mwenye hasira, hususan kwa yule mtu ambaye
alikuambukiza. Unaweza kuwa na wasi wasi kuhusu kuwa na uhusiano wa muda
mrefu au kuwa na watoto. Lakini sio kila mtu huathirika kwa namna hii
anapoambukizwa huu ugonjwa, na hizi hisia haziwezi kubaki moja kwa moja.
Baada ya kisa cha kwanza kikubwa cha ugonjwa wa malengelenge, nilijisikia
kuwa mbali na mwili wangu. Wakati tulipoanza kufanya mapenzi tena, nilikuwa
na wakati mgumu kufikia kileleni au kuamini mwenendo wa hisia zangu. Nilikuwa
nikilia machozi kutokana na hilo tatizo. Nilihisi mwili wangu ulikuwa umevamiwa.
Maumivu yanayotokana na malengelenge hutokea wakati wa hedhi, mfadhaiko
wa kihisia au kimwili, kujamiiana, au kukaa juani. Mara nyingi dalili zake
hazifahamiki. Itakuwa ni rahisi kukabiliana na huu ugonjwa kama utakuwa wazi
kuongelea ukiwa umeshaambukizwa. Kutambua nini kinachosababisha kurudia
rudia kwa ugonjwa na kupunguza shinikizo kwenye maisha yako, kama
unaweza, huweza kupunguza kujirudia rudia kwa huu ugonjwa.
Ugonjwa wa malengelenge unasumbua sana na wenye maumivu, lakini ni kitu
ambacho unatakiwa ujifunze kuishi nacho.
Wakati nahisi uke wangu unaanza kuwasha na kuwa na maumivu, Ni
ukumbusho wa haraka wa kwenda polepole …najaribu kufikiria kupumzika,
kuondoa mawazo na kunywa dawa, kutuliza nguvu eneo lililoathirika. Wakati
mwingine hutaamuli.
TAHADHARI ZA ZIADA ZA KUZUIA KUENEZA UAMBUKIZO WA UGONJWA
WA MALENGELENGE
Hakuna tiba ya ugonjwa wa malengelenge, na jitihada za kutengeneza kinga
dhidi ya ugonjwa huu hazijafanikiwa hadi sasaLicha ya kufanya ngono salama,
epuka kukutana kwa njia yoyote (pamoja na aina yoyote ya ngono) na mtu
mwenye vidonda mdomoni au sehemu za siri, sehemu ambazo kulikuwa na
vidonda hata kama vitakuwa vimeshakauka (bado unaweza kuwaambukiza
wenzi wengine huu ugonjwa hata kama huna vidonda vilivyokuwa wazi). Kama
una homa ya malengelenge au vidonda vya baridi kwenye mdomo au kwenye
kinywa, epuka kufanya ngono ya mdomo. Kama mikono yako imegusa vidonda
vyako, ioshe vizuri, hususan kabla ya kujigusa na kabla ya kugusana. Na kuwa
mwangalifu hasa usiguse macho yako. Epuka pia kujitolea damu au manii
wakati dalili za malengelenge zimeshaonekana.
KUJITIBU MWENYEWE UGONJWA WA MALENGELENGE:
Hakuna ushahidi mwingi wa kisayansi uliofanywa juu ya dawa hizo Pia, matibabu
ambayo huvifanya umajimaj na kulainisha vidonda huvichelewesha kupona.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 38 of 42
Unatakiwa ufanye majaribio ya hapa na pale ili kubahatisha kupata kitu
ambacho kitakuwa na manufaa kwako.
Kituo cha Taifa cha Ugonjwa wa malengelenge (HRC), ambacho kinaendeshwa
na Taasisi ya Afya ya Jamii ya Kimarekani (American Social Health Association
ASHA), hutoa msaada, taarifa, jarida linalotoka mara tatu kwa mwezi linaloitwa
“The Helper”, , na vikundi vya kujiwezesha kwa ajili ya watu wenye ugonjwa wa
malengelenge (tazama “Msaada”).
KUISHI NA VIRUSI VYA HUMAN PAPOLOMA NA UVIMBE SEHEMU ZA SIRI
Kuna aina zaidi ya mia moja ya virusi vya Human papiloma (HPV). Lakini
thelathini tu vinaambukizwa kwa njia ya ngono. Malengelenge sehemu ya siri, ni
uambukizo unaonekana ambao husababishwa na virusi vya Papiloma, na wala
hauhusiani na saratani ya mlango wa mji wa mimba. Hata hiyo, kuwa na aina
yoyote ya virusi vya Papiloma inaweza kumaanisha kuwa umeambukizwa aina
nyingine. Haiwezekani kamwe kutibika, na mengine yanaweza kuwa ni vigumu
kuishi navyo, kutokana na madhara yake. Jali afya yako kwa kwenda kumuona
mtaalam wa afya mara kwa mara, ikiwa ni pamoja na kufanyiwa vipimo vya
kutambua saratani ya kwenye mlango wa mji wa mimba. Pia ni wazo zuri kwako
na wenzi wako kutumia kinga (tazama Sura ya 14, “Ngono salama”).
Malengelenge huweza kutokea tena hata baada ya matibabu, kwa hiyo
yatatakiwa yaondolewe zaidi ya mara moja. Virusi vinaweza kuondelewa eneo la
mwanzo lililoathirika, hata baada ya malengelenge kuondolewa. Huduma
zinapatikana kwenye Taasisi ya Kimarekani ya Afya ya Jamii (tazama “msaada)
MAGONJWA MENGINE YA NGONO
Licha ya maelezo ya magonjwa ya ngono yaliotolewa hapa, kuna mengine
kama homa ya ini aina C, cytomegalovirus (CMV), na molluscum contagiosum.
Kama utakuwa na mahusiano ya kingono ukiwa nje ya nchi ya Marekani au na
mtu mwingine hapa hapa ambaye anatokea nchi nyingine, unaweza
kuambuambukizwa magonjwa ya ngono ambayo sio ya kawaida nchini
Marekani. Magonjwa haya ni pamoja na Lymphogranuloma venereum (LGV),
granuloma inguinale, chancroid, na aina
ya kisonono ambayo ni sugu kutibiwa kwa dawa zinazotumika katika nchi hii.
Baadhi ya magonjwa ya ngono huambukizwa kwa haraka zaidi kwa
ngono ya njia ya haja kubwa. Unaweza
SIDEBAR
kupata uambukizo kwenye njia ya haja kubwa ya ugonjwa wa kisonono,
chlamydia, LGV, kaswende, au malengelenge. Vijidudu vingine vya uambukizo
kama shigella, vinaweza kusababisha kuharisha na tumbo kuuma. Kugusana
kwa mdomo na njia ya haja kubwa pia kunaweza kuambukiza Homa ya ini aina A
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 39 of 42
na giardia, na vimelea vingine vya magonjwa. Ingawa wanawake wengi hufanya
ngono ya mdomoni na njia ya haja kubwa, mtaalam wako wa afya anaweza
asifikirie kukuuliza kuhusu hivi vitendo. Unaweza kupata maelezo zaidi kuhusu
magonjwa ya ngono kwenye mwongozo wa matibabu ya CDC (tazama
“msaada”)
MATIBABU BINAFSI YA MALENGELENGE
DAWA ZA KUTULIZA VIDONDA
JINSI YA KUZITUMIA
Chai ya karafuu, Chai ya rangi
Ponda ponda makokwa ya matunda
madogo ya uvaursi
Pakaa kwenye vidonda.
Tumbukiza kwenye maji (jaza bafu la
kuongea na maji yajae kiasi cha urefu wa
inchi 3-4 - maji ya uvugu vugu na kaa kwa
makalio yako na mapaja tu yakiwa ndani
ya maji; unaweza kupumzisha miguu yako
na mikono kwenye beseni.
Ponda/ saga vidonge vya calcium, mizizi
fulani, au manyoya laini kama ya sungura
na maziwa ya baridi.
Pakaa kwenye vidonda.
Maji maji ya Alovera, dawa ya aina
neosporin, camphor-phenol, povidone
Paaka kwenye vidonda kukausha
MIKAKATI YA KUPUNGUZA AU KUZUIA
UAMBUKIZO WA MALENGELENGE
KUENDELEA.
KWA NINI
JINSI YA
KUTUMIA
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 40 of 42
Epuka vyakula vyenye viwango vikubwa
vya wanga aina argine
Wanga arginine
huchochea virusi vya
malengelenge
Kula kidogo au
usile kabisa.
(Karanga,
chokoleti, wali, ,
na mbegu za
pamba)
Kula vyakula vyenye protini nyingi aina ya
lysine (viazi mviringo, nyama, maziwa,
hamira ya kutengenezea pombe, samaki,
ini, mayai,) au kunywa vidonge vya protini)
Huwazuia virusi
kuendelea kuwa na
nguvu
Ongeza vidonge
vya virutubisho vya
mg. 750-1000
hasa mg. 500 kila
siku kwa ajili ya
kinga
Dawa ya mitishamba (vidonge, chai na
kemikali za pombe)
Hupunguza dalili Au vidonge 2 vya
Echinacea kila
baada ya masaa 3.
kijiko kimoja cha
chai cha tinture
kila baada ya saa
mbili kwenye
vidonda kila siku.
Majani ya kijani (poda), zabibu nyekundu
na majani ya ngano)
Huweza kuwa kinga
ya virusi
Ongezea kwenye
mlo.
Vitamini A,B,C,E; madini ya chuma,
Calcium, na zinki.
Hutoa sumu mwilini,
huongeza nguvu ya
kinga ya mwili, na
kutuliza mishipa ya
neva.
Virutubisho
mbadala vya
vitamini A vya zaidi
ya Iu 10,000
inaweza kuwa ni
sumu
Tibasindano, kwenye miguu. Huongeza mfumo wa
nguvu ya kinga,
hupunguza au kuzuia
dalili.
Bonyeza kwa
nguvu kwa kidole
gumba kati ya
maungio ya
kifundo cha mguu
na unyayo
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 41 of 42
Hili jedwali lina makosa makubwa ya
uchapaji ina bidi kuangalia tena kwenye
kitabu chenyewe kilivyo pangilia haya
maelezo
UAMBUKIZO WA NJIA YA MKOJO USIOSABABISHWA NA BAKTERIA WA
KISONONO:
Uchafu wowote kutoka kwenye njia ya mkojo ambao hausababishwi na ugonjwa
wa kisonono huitwa uambukizo wa njia ya mkojo usiosababishwa na ugonjwa
zinaa (NGU). Istilahi hii mara nyingi
huusu maambukizo kwa wanaume. Huu sio tafsiri kamili ya utambuzi
kimatibabu. Uambukizo unaweza kusababishwa na vimelea vya wadudu wa
aina ya chlamydia, ureaplasma, urealyticum, (ambao hupatikana kwa watu
wengi wasioonyesha dalili), au micoplasma genitalium. Magonjwa haya huweza
kusababisha ugonjwa wa mlango wa mji wa mimba, Ugonjwa wa uvimbe wa via
vya uzazi, utasa, kutoka kwa mimba, na kujifungua kabla ya muda, kwa hiyo
mwanamke mwenye utasa au historia ya kutoka kwa mimba anaweza
akafanyiwa vipimo vya magonjwa haya.
MASUALA YA KIJAMII NA KISIASA:
Kujikinga dhidi ya uambukizo ni jambo la haraka sana, kwa sababu virusi na
magonjwa ya zinaa yasiyotibika vinaendelea kuongezeka . Hata magonjwa ya
ngono yanayotibika yanaweza kuleta madhara makubwa kiafya kama
hayatagunduliwa mpema. Licha ya hivyo, Unyanya paaji wa kijamii unaohusiana
na magonjwa ya ngono huweza kuwa ni kikwazo katika kupata huduma
tunayoihitaji. Watu wengine bado wanaamini kwamba magonjwa ya ngono ni
adhabu kwa wanaofanya ngono isiyo isivyostahili/ halali .
Hadi hivi karibuni, shule za madaktari zilikuwa
zina puuzia magonjwa ya ngono. Hata hivi leo wataalam wa afya wana weza
wakawa wamepata mafunzo kidogo ya kufanya uchunguzi na kutibu magonjwa
ya ngono, hususan kama hakuna dalili zozote.
Magonjwa Yanayoambukizwa Kwa Njia Ya Ngono (“Sexually Transmitted Infections”).
For more information, see: http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania
Page 42 of 42
TUNAHITAJI KINGA BORA ZAIDI
Wanawake mahali popote wanahitaji kupata dawa za uzazi wa mpango nas
dawa za za kujikinga na magonjwa ya ngono zinazofanya kazi. Wanawake tuko
katika hatari kubwa zaidi kuliko wanaume kutokana na sababu za kiutamaduni,
kiuchumi, na kibaiolojia, kwa hiyo kutulinda kunatakiwa kupewe kipaumbele
kikubwa Wanaharakati wa masuala ya afya za wanawake wanafanya kazi
yakuhamasiha kuwepo na maendeleo ya kutengeneza dawa za kuua vimelea
vya magonjwa ambavyo vina weza hupakwa moja kwa moja ukeni au kwenye
sehemu ya haja kubwa ambayo huzuia au kupunguza hatari ya kueneza
maambukizi. Hata hivyo, kemikali nyingi ambazo huweza kuua vijidudu vya
magonjwa ya ngono hazitengenezwi kuwa dawa kwa sababu hakuna fedha za
kutosha, na makampuni ya kutengeneza dawa huweka kupata faida mbele
kwanza. Utafiti pia wa kufanyia majaribio dawa ambazo zinatazamiwa kutofanya
kazi umekuwa ukipunguzwa kasi kutokana na sababu za kimaadili.
TUNAHITAJI ELIMU NA HUDUMA ZA MAGOJWA YA NGONO
Hata kama viwango vya magonjwa ya ngono miongoni mwa vijana wa
kimarekani ni vikubwa kuliko kwenye nchi nyingi zilizoendelea, hakuna
msukumo wa kutosha wa kisiasa kuboresha elimu na kinga. Msukumo kutoka
kwenye vikundi vya kidini unaopinga elimu ya ngono na usambazaji wa mipira ya
kiume-kondom umekuwa ni kikwazo katika jitihada za kuzuia maambukizi,
hususan mashuleni na kwenye kliniki zinazotumiwa na vijana na wasichana.
Tafiti zinaonyesha kwamba, taarifa sahihi za ngono hazichangii kuongezeka kwa
vitendo vya ngono miongoni mwa vijana, na kwamba magonjwa ya ngono
yanaweza kuzuiwa. Programu za elimu ya magonjwa ya ngono katika mashule
zinaweza kuwa nzuri kama zinaungwa mkono. Usambazaji wa mipira ya kiume
umethibitisha kuwa ni kinga imara. Shule ambazo hugawa mipira ya kiume kwa
wanafunzi wake zimeripoti matukio machache ya kujamiiana kwa wanafunzi
ukilinganisha na shule ambazo hazina programu hii, na kuongezeka kwa
kiwango cha kufanya ngono salama. Licha ya hiyo, kwa sababu ya hisia za wa
jamii ,mabadiliko hutokea taratibu na suala la fedha pia huwa ni kikwazo na
wakati mwingine hukwamisha kabisa. Kwa hiyo hatuna budi kuendelea kufanya
kwa haraka kutoa elimu sahihi inayolingana na tamaduni ya kujikinga na
matibabu kwa watu wote.
No comments:
Post a Comment